Psalms 37:1-4

Mwisho Wa Mwovu Na Urithi Wa Mwenye Haki

Zaburi ya Daudi.

1 aUsisumbuke kwa ajili ya watendao maovu,
wala usiwaonee wivu watendao mabaya,
2 bkwa maana kama majani watanyauka mara,
kama mimea ya kijani watakufa mara.

3 cMtumaini Bwana na utende yaliyo mema;
Kaa katika nchi ukafurahie malisho salama.
4 dJifurahishe katika Bwana
naye atakupa haja za moyo wako.
Copyright information for SwhNEN